Vyakula vya kuku vinaweza kupatikana madukani au kutengenezwa na mfugaji mwenyewe. Ili kuku aweze kukua haraka na kutoa mazao mengi na bora ni lazima chakula kitengenezwe katika mchanganyiko wenye uwiano mzuri uliopendekezwa.
Chakula
cha kuku ni lazima kiwe na viinilishe muhimu kama vile protini, wanga, madini
na vitamini. Hakikisha chakula unachotengeneza kina mchanganyiko ufuatao:
·
Vyakula vya kujenga mwili kama vile jamii ya kunde, samaki,
dagaa, mashudu ya ufuta, pamba na alizeti
·
Vyakula vya kulinda na kukinga mwili usipate maradhi kama vile
mafuta ya samaki na majani mabichi kama kabichi, mchicha, majani ya mpapai na
nyasi mbichi
·
Vyakula vinavyojenga mifupa kama vile aina ya madini, chokaa,
mifupa iliyosagwa na chumvi. Ukosefu wa vitamini na madini kama Kalishamu na
Fosiforasi husababisha matege, kukunjamana kwa vidole, kufyatuka kwa misuli ya
goti na kupofuka macho.
Maji ni
muhimu sana kwani husaidia kulainisha na kurahisisha usagaji wa chakula, na
kupunguza joto. Wakati wa joto kali kuku wapewe maji mengi.
Kabla
ya kutengeneza chakula lazima mtengenezaji ajue haya:
·
Jinsi ya kupata vyakula vya aina mbali mbali
·
Kiasi cha viinilishe vinavyohitajika kwa kuzingatia umri na aina
tofauti ya kuku; kwa mfano vifaranga wanahitaji protini asilimia 18 hadi 22,
kuku wanaokua asilimia 17 hadi 19 na kuku wa mayai asimilia 15 hadi 17. Vile
vile madini aina ya Kalishamu kiasi cha asilimia tatu hadi nne kinahitajika kwa
kuku wa mayai na asilimia moja kwa kuku wa nyama na vifaranga.
·
Viwango vya uchanganyaji wa aina za vyakula mbali mbali. Ili
mtengenezaji aweze kutengeneza chakula bora ni muhimu afuate kiwango cha
uchanganyaji
Kilichopendekezwa.
Kiasi cha aina moja ya chakula kinapozidi kinaweza kuleta madhara.
Jedwali
lifuatalo linaonesha kiwango kinachotakiwa kwa baadhi ya vyakula.
1.
Vyakula na viwango vinavyohitajika kwa asilimia 100
Aina ya Chakula |
Kiwango cha
uchanganyaji (%) |
||
Vyakula |
Vifaranga |
Kuku wa nyama |
Kuku wa mayai |
Mahindi |
70 |
70 |
70 |
Ulezi |
20 |
40 |
40 |
Mtama |
20 |
30 |
30 |
Mpunga |
40 |
70 |
70 |
Ngano |
5 |
40 |
40 |
Pumba za mahindi |
10 |
20 |
20 |
Pumba za mpunga |
10 |
20 |
20 |
Pumba za mtama |
10 |
20 |
20 |
Pumba za ngano |
5 |
15 |
15 |
Mashudu ya nazi |
10 |
30 |
40 |
Mashudu ya pamba |
5 |
10 |
5 |
Mashudu ya alizeti |
10 |
20 |
20 |
Mashudu ya ufuta |
10 |
10 |
5 |
Damu iliyokaushwa |
5 |
5 |
5 |
Mifupa iliyosagwa |
5 |
5 |
7.5 |
Dagaa |
10 |
5 |
5 |
Lusina iliyosagwa |
– |
– |
– |
(Lucerne meal) Lukina |
5 |
5 |
5 |
Lcuecana meal |
2.5 |
5 |
5 |
Chokaa |
5 |
5 |
5 |
Chumvi |
0.5 |
0.5 |
0.5 |
Soya |
10 |
20 |
20 |
·
Kuhusu kiasi cha viinilishe kama protini, wanga, madini na
vitamini vilivyomo kwenye aina za vyakula vitakavyochanganywa, Mfugaji
anashauriwa amuone mtaalamu wa mifugo aliyekaribu naye aweze kumpa ushauri
zaidi.
·
Mchanganyiko uwe na zaidi ya aina moja ya vyakula kwa mfano
vyakula vya kujenga mwili vitokanavyo na wanyama na mimea.
1.
Mfano wa kutengeneza kilo 100 za chakula cha kuku;
Vyakula |
Kiasi (Kg) |
Mahindi |
30.00 |
Pumba za mahindi |
20.00 |
Soya |
18.00 |
Mashudu ya alizeti |
20.50 |
Dagaa |
5.00 |
Mifupa iliyosagwa |
4.00 |
Chumvi |
0.50 |
Vitamini |
2.00 |
Jumla |
100.00 |
1.
Mfano wa chakula cha kukuzia kuanzia juma la nne hadi la nane
Vyakula |
Kiasi (Kg) |
Mahindi |
45.00 |
Pumba za mahindi |
20.00 |
Mashudu ya pamba |
5.00 |
Soya |
20.00 |
Dagaa |
2.50 |
Mifupa iliyosagwa |
5.00 |
Chumvi |
0.50 |
Vitamini |
2.00 |
Jumla |
100.00 |
1.
Mfano wa chakula cha kuku wa mayai kuanzia juma la nane hadi la
ishirini
A |
B |
||
Vyakula |
Kiasi (Kg) |
Vyakula |
Kiasi (Kg) |
Mahindi |
45.00 |
Mahindi |
45.00 |
Pumba za mahindi |
25.00 |
Pumba za mahindi |
30.00 |
Soya |
5.00 |
Soya |
5.00 |
Mashudu ya alizeti |
10.00 |
Mashudu ya pamba |
5.00 |
Dagaa |
4.00 |
Dagaa iliyokaushwa |
4.00 |
Damu |
3.00 |
Mifupa iliyosagwa |
2.50 |
Chokaa |
3.00 |
Chokaa |
3.00 |
Chumvi |
0.50 |
Chumvi |
0.50 |
Vitamini |
2.00 |
Vitamini |
2.00 |
Jumla |
100.00 |
Jumla |
100.00 |
1.
Mfano wa chakula cha kuku wa mayai kuanzia wiki ya ishirini na
kuendelea
A |
B |
||
Vyakula |
Kiasi (Kg) |
Vyakula |
Kiasi (Kg) |
Mahindi |
50.00 |
Mahindi |
40.00 |
Pumba za mahindi |
15.00 |
Pumba za mahindi |
25.00 |
Mashudu ya pamba |
5.00 |
Mtama |
5.00 |
Soya |
18.00 |
Mashudu ya alizeti |
10.00 |
Dagaa |
4.50 |
Dagaa |
4.00 |
Mifupa iliyosagwa |
3.00 |
Damu iliyosagwa |
5.00 |
Chokaa |
2.00 |
Mifupa iliyosagwa |
4.50 |
Chumvi |
0.50 |
Chokaa |
4.00 |
Vitamini |
2.00 |
Chumvi |
0.50 |
Jumla |
100.00 |
Vitamini |
2.00 |
|
|
Jumla |
100.00 |