ZoyaPatel

Wawili Wapatikana Wamefariki Katika Sehemu ya kuhifadhia mizigo ya Ndege

SohaniSharma

 


Fort Lauderdale, Florida: 

Miili ya watu wawili imegunduliwa katika sehemu ya magurudumu ya ndege ya shirika la JetBlue iliyotua katika Uwanja wa Ndege wa Fort Lauderdale-Hollywood, Florida, ikitokea Uwanja wa Ndege wa JFK, New York.

Kwa mujibu wa taarifa za shirika hilo, miili hiyo iligunduliwa Jumatatu jioni, Januari 6, wakati wa ukaguzi wa kawaida wa matengenezo baada ya safari ya ndege.

JetBlue ilitoa taarifa kwa vyombo vya habari ikisema:
"Jumatatu jioni, Januari 6, katika Uwanja wa Ndege wa Fort Lauderdale-Hollywood, watu wawili waligunduliwa katika sehemu ya magurudumu ya moja ya ndege zetu wakati wa ukaguzi wa kawaida baada ya safari. Kwa masikitiko makubwa, wote walikuwa wamefariki."


Hadi sasa, haijajulikana kwa namna gani wa watu hao waliweza kuyafikia magurudumu ya ndege hiyo.

JetBlue imesema inashirikiana kwa karibu na mamlaka husika kusaidia katika uchunguzi wa tukio hili.

"Tukio hili ni la kusikitisha sana, na tumejitolea kushirikiana kwa ukamilifu na mamlaka ili kuelewa kilichotokea," JetBlue iliongeza

Mamlaka za usalama wa anga zinaendelea kuchunguza tukio hili ambalo limezua maswali kuhusu usalama wa ndege na jinsi watu walivyoweza kuingia katika sehemu ya magurudumu bila kugunduliwa.

Ahmedabad
Hyderabad
Previous Post Bangalore Next Post

نموذج الاتصال