ZoyaPatel

Dkt. Mpango afunguka kwa mara ya kwanza sababu iliyomsukuma kustaafu

SohaniSharma

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip Isdor Mpango, ametaja umri, kufanya kazi muda mrefu serikalini na uwepo wa vijana wanaoweza kumsaidia Rais katika Majukumu ya Nafasi ya Makamu wa Rais ni kati ya sababu ambazo zimemsukuma kuomba kustaafu nafasi hiyo.

Akizungumza leo katika kikao kazi cha Tano cha Serikali Mtandao, kinachofanyika ukumbi wa Kimataifa wa AICC jijini Arusha, Dkt. Mpango amesema

“Kwa mujibu wa Takwimu za Sensa ya watu na Makazi ya Mwaka 2022, asilimia 77 ya idadi ya watu nchini ni vijana; sasa Mimi nimetumika serikalini kwa muda wa kutosha ….. bado nina nguvu, yapo mambo ambayo ninaamini kwamba inahitaji nafasi kwa ajili ya kuchangia pato na maendeleo ya Taifa.

Makamu wa Rais ameongeza kuwa nafasi adhimu alizowahi kutumika serikalini zinaweza kutumikiwa na watanzania wengine, hivyo uamuzi wake unalenga pia kuacha nafasi ya watu wengine kutoa mchango kwa Taifa hasa kwa nafasi alizohudumu.

“Ukipanda Treni ni muhimu kujua unapandia kituo gani, muda gani na unateremka muda gani na kituo gani; la sivyo litakupitiliza. “Ninaamini kuwa chaguo lililofanywa na chama chetu ni chaguo sahihi kabisa” amesema Dkt. Mpango.

Dkt. Mpango amehudumu serikalini kwa nafasi mbalimbali ikiwemo Mkufunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa miaka 14, Naibu Katibu Mkuu Hazina, Katibu Mtendaji Tume ya Mipango kwa Miaka sita (6), Waziri wa Fedha, Miaka mitano na miezi minne, Benki ya Dunia, Msaidizi wa Rais Kikwete - Ikulu, na miaka minne, akiwa Makamu wa Rais wa Tanzania katika serikali ya Awamu ya Sita.

Amehimiza viongozi wengine kuona umuhimu wa kuwa na muda wa kutosha kuandika, ili kujenga kumbukumbu nzuri na historia ya Taifa la Tanzania.


Ahmedabad
Hyderabad
Previous Post Bangalore Next Post

نموذج الاتصال