ZoyaPatel

Kamonga aomba mwarobaini wa kukatika kwa umeme maeneo ya uzalishaji Ludewa

SohaniSharma

 


Mbunge wa Ludewa, Joseph Kamonga leo Februari 10, Bungeni jijini Dodoma ameitaka serikali kutenga bajeti ya kutosha ili kuhakikisha maeneo yenye uzalishaji katika Wilaya ya Ludewa yanapata umeme wa kutosha ili kuondokana na adha ya kukatika kwa umeme na hivyo kuathiri shughuli za uzalishaji.

Kamonga ameelekeza swali kwa Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ambaye amekiri uwepo wa tatizo hilo huku akiweka bayana kuwa serikali mwanzoni ilifanikiwa kutuma wataalamu kwa ajili ya kufanya uhakiki pamoja na gharama itakayotumika kwa ajili ya kubadilisha miundombinu.

Naibu Waziri amemhakikishia Mbunge Kamonga kuwa serikali itaendelea kutafuta fedha kwaajili ya kufanya marekebisho katika maeneo ya uzalishaji ili wananchi wa Ludewa waendelee kuwa sehemu ya wanaufaika wa umeme kupitia uzalishaji wao.

Ahmedabad
Hyderabad
Previous Post Bangalore Next Post

نموذج الاتصال