ZoyaPatel

Mwabukusi – TLS Tunaposhirikiana na Serikali hatulambi asali

SohaniSharma



Rais wa Chama cha wanasheria wa Tanganyika (TLS) Boniface Mwabukusi ameshauri serikali na sekta binafsi kuendelea kushirikiana katika kusimamia na kutekeleza sheria mbalimbali zilizowekwa ili kuongeza ufanisi katika kuwahudumia watanzania.

Mwabukusi ametoa kauli hiyo leo Februari 3 ikiwa ni kilele cha maadhimisho ya wiki ya Sheria duniani.



Katika Hafla hiyo inayofanyika jijini Dodoma, Mgeni Rasmi akiwa Rais wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, Mwabukusi amenukuliwa akisema “ Tunaposhirikiana na serikali hatulambi asali….TLS sio kikundi cha magaidi ….. sehemu ya kuonya tutaonya kwa haki, kupongeza tutapongeza kwa haki na yale ya kushiriki kufanya kazi tutashiriki kwa haki kulijenga taifa letu na kumhudumia mwananchi” amesema.

Pia amesisitiza kwa kusema “TLS tumekuwa tukizunguka kupitia Mama Samia Legal Aid, na sisi tumekuwa tukishiriki mikoa yote kuwafikia wananchi; kwahiyo kuptia program kama hiyo serikali inakuwa inatusaidia moja kwa moja kwa sababu wananchi wengi wanaofikiwa na huduma ile ni wale wananchi ambao hawana uwezo wa moja kwa moja wa kupata ile huduma ya mawakili kulingana na uwezo wao kiuchumi na maeneo waliko”



Mwabukusi ameshauri sheria zinazotungwa, ziwe na ushirikishaji wa maoni baina ya watunga sheria na wananchi ambao ndio watumiaji wa sheria hizo.

Mbali na hayo ameshauri kuboreshwa kwa maslahi ya mahakimu kwa kile alichoeleza wao ndio wanaoshughulika na wananchi wa chini; hivyo kutokuwepo kwa maslahi mazuri kunaweza kuwa chanzo cha upindishwaji wa haki za wananchi.

Ahmedabad
Hyderabad
Previous Post Bangalore Next Post

نموذج الاتصال