ZoyaPatel

Zitto Kabwe aibukia sakata la Trump kusitisha misaada Afrika

SohaniSharma

Mwanasiasa na Kiongozi Mstaafu wa Chama cha ACT Wazalendo Zitto Kabwe amesema uamuzi wa Trump kusitisha misaada dhidi ya nchi za Afrika una uhusiano wa moja kwa moja na kuokoa uchumi wa Taifa lake na kurejesha nguvu, kwa kile alichoeleza tishio la ukuaji kwa kasi wa uchumi wa China.

Zitto Kabwe akipiga stori na Power Breakfast ya Clouds FM leo Februari 12, amesema kuwa hakuna shaka kuwa kwa sasa China ni Taifa lenye nguvu kubwa duniani ila kinachoitofautisha na mataifa ya Magharibi kama Marekani ni kuwa China haipendi kuingilia mataifa mengine.

Ametumia ishara mbalimbali ikiwemo kukua na kujitosheleza kwa uchumi wa Taifa la China, nguvu ya kijeshi na Diplomasia iliyopanuka kuwa sababu za kuifikiria kwa ukubwa huo.

China limekuwa ni Taifa ambalo lipo kwenye fikra za wanasiasa wengi wa Marekani kwa sababu ya kasi yao ya ukuaji wa uchumi, namna wanavyoshikLria mnyororo wao wa ugavi, na sasa tunazungumzia ukuaji wa teknolojia ambayo imewekezwa kwa kiasi kikubwa na uwepo wa madini mkakati, na hivyo kuwa na bidhaa kama magari ya umeme, na malighafi mbalimbali, hiyo ndio sababu Marekeni na mataifa ya Ulaya yanafanya kila njia kuanzisha sera za uwekezaji ambazo zinambana China. Amenukuliwa Zitto Kabwe

Ameongeza kuwa usitishaji wa misaada Barani Afrika na kwingineko duniani utakuwa na athari ya moja kwa moja kwa Marekani kupoteza ushawishi.

Leo hii Marekani akija Tanzania na ana jambo lake ana kipi cha kushawishi ikiwa hatoi msaada wowote ..Marekani ameacha mlango wazi hivyo China ataingia na kuleta hata modeli yake ya Demokrasia kwa sababu atakuwa na hiyo nguvu ambayo Marekani aameipoteza. Amesema Kabwe

Ahmedabad
Hyderabad
Previous Post Bangalore Next Post

نموذج الاتصال