ZoyaPatel

Njombe RRH FC kushuka dimbani Jumamosi, Sokoine dhidi ya Hospitali ya Kanda Mbeya (MZRH FC)

SohaniSharma

 

Klabu ya Soka ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe, (Njombe RRH FC) inatarajia kuingia dimbani dhidi ya Timu ya Soka ya Hospitali ya Kanda Mbeya (MZRH FC) Mchezo unaotarajiwa kuchezwa mnamo Aprili 5, Jumamosi katika Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya.

 

Akizungumza jana Aprili Mosi, baada ya mazoezi ya kuendelea kujiweka imara Kocha wa Njombe RRH FC, Admin Mashaka amesema anatambua ukubwa wa Timu ya Hospitali ya Kanda Mbeya lakini wamejipanga kuhakikisha wanarudi na ushindi katika mchezo huo wa Ugenini.

 

Naye Nahodha wa Timu ya Njombe RRH FC Peter Mwanjabala, amepongeza mwitikio wa wachezaji, wapenzi na mashabiki wa Timu hiyo kwa kuendelea kujitokeza katika michezo ambayo imekuwa ikiendelea ili kujifua zaidi kuelekea mchezo huo.

 

Amewataka mashabiki kuendelea kuchangia nauli ili kuongeza nguvu ya mashabiki wa Njombe RRH FC watakaojitokeza kuipa nguvu timu hiyo, huku akiahidi kuwa timu hiyo itajitahidi kurudi na ushindi.

 

Kwa upande wake Afisa Michezo wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe, akizungumza pia kwa niaba ya Menejimenti ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe amesema kumekuwepo na ushirikiano mzuri na udugu wa kudumu kati ya Hospitali hii na Hospitali ya Kanda Mbeya ikiwemo kuwajengea uwezo watumishi wa Njombe RRH, hivyo uwepo wa mchezo huo ni mwendelezo wa ushirikiano na kufahamiana miongoni mwa watumishi wa taasisi hizi mbili.

 

Pia ameushukuru Uongozi wa Hospitali kwa kuipa nguvu timu hiyo kwa kufanya uwezeshaji katika maeneo mbalimbali yatakayosaidia kufanikisha uwepo wa mchezo huo.

 

Ahmedabad
Hyderabad
Previous Post Bangalore Next Post

نموذج الاتصال