ZoyaPatel

Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan azindua Benki ya Ushirika Tanzania Jijini Dodoma

SohaniSharma

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema uanzishwaji wa Benki ya Ushirika Tanzania ni utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi na utekelezaji wa wazo la muda mrefu la kuhakikisha sekta ya ushirika inakuwa na benki kubwa inayoihudumia.

 Rais Dkt. Samia ameyasema hayo leo wakati akizindua Benki ya Ushirika Tanzania, katika Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete jijini Dodoma.

Benki hiyo itakayojikita kuchochea ufadhili wa mitaji zaidi kwenye sekta ya ushirika inamilikiwa kwa 51% na vyama vya ushirika, 20% na Benki ya CRDB, 10% na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na 9% na wanahisa wengine.

Rais Dkt. Samia ameipongeza benki hiyo kwa kuanza vizuri ambapo amesema “Mmeanza na mtaji wa Shilingi Bilioni 58, ni mtaji mkubwa, benki haianzi kinyonge. Kiasi hiki kitasaidia kuongeza mitaji kwa wakulima kwa kutoa mitaji na kuchochea kuongezeka chakula na mazao mengine ya kilimo nchini."

Aidha, Mhe. Rais Dkt. Samia amebainisha kuwa dhamira ya Serikali ni kuona ushirika unaimarika na kuongeza mchango wake kwenye Pato la Taifa na kukuza uchumi wa nchi kwa ujumla.

Katika hatua nyingine, Mhe. Rais Dkt. Samia amezitaka Wizara ya Fedha, Wizara ya Kilimo kwa kushirikiana na Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kutafuta jawabu la changamoto ya upatikanaji mitaji katika sekta ya kilimo nchini. Vilevile, Rais Dkt.

 Samia ameiagiza Tume ya Maendeleo ya Ushirika kusimamia vyama vya ushirika ili vijiendeshe kibiashara na kuvitaka vyama vyote nchini kuimarisha uwajibikaji na uwazi.

Ameeleza kuwa matumizi ya TEHAMA katika uendeshaji wa ushirika, yatasaidia kujenga imani ya wanaushirika kwa vyama vyao.








Ahmedabad
Hyderabad
Previous Post Bangalore Next Post

نموذج الاتصال